Story

Don't have an account yet? Sign Up Now. It's free!

The Lausanne Global Conversation is on the World Wide Open Network

Blog

  • Print
  • PDFPDF
  • Flag

sera za lugha zinazotakikana kanisani, Afrika.

Author: Jim Harries
Date: 02.06.2010
Category: Partnership, Truth and Pluralism, Leadership Development

Rate (0)
  • Currently 0.00/5
Favorite (0) Recommend

Translations

Available Translations:

Originally Posted in English

Siku moja nikiwa Zambia, nilipokuwa mwalimu wa shule ya upili, niliweka tangazo fulani kwa sehemu ya taarifa za shule. Baada ya siku mbili nilipitia hapo na Walimu wenzangu Wazambia wawili.  Niliona mtu mwingine alishafunika karatasi yangu kwa kuweka karatasi yake juu ya yangu.  Nilivyowaelezea wenzangu, wakacheka.  Nilifikiri – kwa nini wanacheka kwa kitendo kibaya kama kile?  Niligundua kwamba hata ukitumia lugha moja, bado jinsi inatumiwa inaweza kuwa tofauti. (Kwetu Ulaya mtu hangalicheka, angalisema pole na jinsi inatakikana hali irekebishwe.)

Nilipofika Zambia mara ya kwanza, nikaanza miradi mbali mbali ya ukulima hapo shuleni. Wazambia wenzangu walifurahie kuona maendeleo shambani.  Lakini pia ilionekana kwa ufahamu wao ya kwamba miradi itaendeleo tu nikiwepo au Mzungu mwingine akija kuiendeleza.  Nilianza kuona hio dalili mahali popote nilipoenda.  Nilitafuta piki piki ili nitembee nifanye uchunguzi zaidi.  Sio miradi yangu midogo shuleni tu, lakini miradi mikubwa katika sehemu mbali-mbali ilikuwa inafanya kwa muda kidogo, lakini Wazungu walipoondoka miradi ikaanguka.  Kufungwa kwa miradi yote hapa KIST mwaka uliopita (2005) inaonyesha hali ile ile ngumu pia hapa Kenya.

Watu hupenda kutoa sababu mbali mbali kueleza kutofaulu kwa miradi. Wengine husema ni ukosefu wa rasilmali. Huu ni ngumu kuamini vile pesa nyingi imemwagwa kwa bara ya Afrika na shirika mbali mbali za misaada.  Wengine hutaja bahati mbaya, ufisadi, vifo vingi, hali ya hewa, kuwepo vita, ukosefu ya elimu n.k.  Lakini sababu aina hizo kweli zinaharibu hii miradi yote? Hali ingine ya msingi inajificha na maneno aina hayo. Kwa nini miradi ya kuendeleza uchumi wa Kiafrika mara nyingi inakwama?

Tuangalie upande wa kanisa.  Siku moja nilipokuwa Zambia niliambiwa ‘Mwafrika hawezi kuhubiri vile Mzungu anayehubiri.’  Baada ya miaka kadhaa nilipokuwa Kenya niliambiwa ‘Mzungu hawezi kuhubiri kama Mwafrika.’  Nilipuuza kwanza.  Inawezekanaje Mungu kutofanya kwa njia sawa na hawa wote?  Baada ya muda hapa Kenya, nilitambua ni kweli.  Pengine sio haiwezekani kabisa, lakini ni ngumu sana. Tena inafanywa kupitia kwa uigaji. Nimeona pia Mwafrika akienda kuhubiri Ulaya. Waingereza hushangaa kwa urahisi; sio rahisi kuyafahamu maneno yake. Hapa Afrika mara nyingi Watu wanakuwa tayari kulisikiliza Neno la Mzungu ikiwa Mhubiri anatumia lugha ya pesa. Pesa isipokuwepo kugawanya wakati ule anapohubiri, lazima asisitize maneno yake kupitia kwa mali yake kwa njia ngine. Wacha ajaribu kazi yake bila ugawanyaji ya fedha na bila kutumia lugha ya ugeni ambayo inataminikwa, na tuone.

Badala ya kusaidia, mara kwa mara mhubiri mgeni Mzungu analeta vita na ugawanyiko kanisani.  Anawapa watu uamuzi ngumu – fuata Mungu na umaskini, au tii maneno yake na pokea mali.  Haya yamewaangusha watumishi wengi wa ukweli wa Mungu.  Huo ni uharibifu moja unaotokea tukimruhusu mgeni kutumia mali yake kulazimisha maneno ambayo hayalingani na mila inayolengwa.

Mara nyingi nimejikuta katikati ya shida hii.  Maana yake; mgeni kutoka Ulaya anaongea na kiongozi wa kanisa hapa Kenya, nikiwa ninasikia.  Mgeni huyu Mzungu anavyoongea, ninayafahamu shabaha yake sababu mimi pia nimetoka mahali ametoka.  Ninagundua pia vile Mwafrika akimsikia anakosa kumfahamu barabara.  Halafu Mwafrika akiongea (tuseme anatumia Kiingereza pia) ninaweza fahamu kitu anacholenga zaidi ya huyu Mzungu sababu nimeishi hapa kwa miaka nyingi.  Lakini jibu la Mzungu linaonyesha kukosa kufahamu kwake.  Hivyo ndivyo mijadala inaendelea.

Keywords: Kiswahili, Lugha, uhusiano, injili, mataifa

Conversation Post Comment

There are not currently any comments.

You must be logged in to post a comment. If you don’t have an account, you can sign up now (it’s free and easy!).